Waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Wahoji Kuhusu Afya ya Askofu Gwajima

Waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, wamesali Jumapili ya tatu bila kuwapo kwa Askofu wao, Josephat Gwajima,lakini wameshtushwa na taarifa kuwa kiongozi huyo wa kiroho ni mgonjwa na anapata matibabu nje ya nchi. 


Waumini hao walisema wamekuwa wakisikia kuwa askofu wao anatafutwa na Jeshi la Polisi na juzi wamesikia kuwa anapata matibabu nje ya nchi wakati wao hawajatangaziwa rasmi kuhusu taarifa hizo. 


Juzi, Wakili wa Askofu Gwajima, Peter Kibatala aliileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa mteja wake hakufika mahakamani kwa kuwa yuko nje ya nchi kwa ajili ya matibabu. 


Askofu Gwajima alitakiwa kufika mahakamani hapo anakokabiliwa na kesi ya kumtolea lugha chafu Askofu Mkuu Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo inayosikilizwa na Hakimu Mkazi, Cyprian Mkeha. 


Mbali na taarifa za kuumwa, pia Gwajima anatafutwa na Polisi baada ya kusambaa kwa sauti inayosikika kama yake ikitaka Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete afikishwe mahakamani kwa yote yaliyofanyika katika utawala wake. 


Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema jana kuwa atalizungumzia suala hilo leo Jumatatu. 


Katika ibada ya jana, kama kawaida, Mchungaji Adriano Edward hakuwaeleza chochote waumini wa kanisa hilo kuhusu alipo Askofu Gwajima wala hali ya afya yake. 


Mchungaji Adriano alipotakiwa kuzungumzia suala la afya ya Gwajima, alisema kupitia msaidizi wake kuwa hawezi kuzungumza chochote na vyombo vya habari. 
Habari zilizopo katika Magazeti ya Leo Jumatatu July 04, 2016  


Vibonzo:Katuni bora zaidi leo Jumatatu July 04, 2016 Bofya hapa 

LOWASSA APIGIWA SALUTI NA WANAJESHI LEO JUMAPILI JULY 03, 2016  Bofya hapa
CHADEMA Waapa Kutibua Mkutano wa CCM ,Vijana 2000 Kupelekwa Dodoma Kwa Ajili ya Kazi Hiyo Bofya hapa 

 Video:Chadema kuzuia Mkutano wa CCM wa kuchagua mwenyekiti wa chama Bofya hapa
Habari zilizopo katika Magazeti ya leo Jumapili July 03, 2016 Bofya hapa


Vibonzo: Katuni tano bora zaidi leo Jumapili July 03, 2016 Bofya hapa

TFF wajichanganya kwa Muro bofya hapa

Tamko la RC Makonda kuhusu mashoga waliopo jijini Dar es Salaam 


 Hatimaye TAKUKURU na TRA Wamtaja Mtu Aliyekuwa Akiibia Serikali Milioni 7 Kwa Kila Dakika Bofya hapa

 Ufafanuzi wa TRA kuhusu ongezeko la thamani kwenye huduma za kifedha Bofya hapa









Like page yetu ya facebook upate habari kwa urahisi na haraka zaidi BOFYA HAPA

Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top