KAULI YA KWANZA YA GUARDIOLA BAADA YA KUTAMBULISHWA MANCHESTER CITY

Kocha mpya wa Manchester City Pep Guardiola amesema kwamba ameamua kuja Ligi Kuu ya England ili kuthibitisha ubora wake

Jana idadi ya mashabiki takriban 7,000 walijitokeza kwenye uwanja wa Etihad Stadium kumsikiliza Guardiola akiongea kwa mara ya kwanza kama meneja wa Manchester City.

“Ndio maana nipo hapa. Nimethibitisha ubora wangu nikiwa na Barcelona, nimefanya hivyo nikiwa Ujerumani na Bayern Munich na sasa nataka kuthibitisha na England.” Guardiola amesema.

Siwezi kufanikisha hilo peke yangu. Nahitaji wachezaji, viongozi. Tunahitaji mashabiki. Bila ya hayo yote, kamwe hatutafanikiwa.

Mhispania huyo amejiunga na City akitokea Bayern Munich ambapo kwa miaka mitatu aliyodumu klabuni hapo amewapa ubingwa wa Bundesliga mara tatu licha ya kushindwa kufika hata mara moja fainali ya Klabu Bingwa.

Hata hivyo, kiungo huyo wa zamani wa Uhispania alishinda kombe hilo mara mbili wakati akiwa na Barcelona

Anaamini kwamba ushirikiana bora na kujituma ndio siri kubwa ya mafanikio mwenye timu.

Napenda wachezaji ambao hawajifikirii wenyewe tu bali wanafikiria muda wote juu ya timu (Manchester City),” amesema Guardiola.

“Sisi sote tunafanya kazi hapa kwa ajili ya timu. Sababu kubwa ya kuwa hapa ni kufanya kila linalowezekana kuifanya klabu yetu iwe bora.”

“Sihitaji watu ambao wana fikra za kutaka klabu iwafanyie wao mambo. Sote tuko hapa kuifanya Manchester City kuwa klabu bora kuelekea miaka mitatu au minne ijayo.”

Aliongeza: “Moja ya sababu zilizopelekea mimi kuja Manchester City ni kuwa na ufahamu juu ya (Mkurugenzi wa Michezo) Txiki Begiristain namna anavyothamini uwepo wa wachezaji vijana kuanzia umri wa miaka 13, 14, 15, 16, 17 na kuendelea. Hawa wanakuwa kwenye misingi ya timu na baadaye kuungana na sisi kwenye kikosi cha wakubwa.”
Habari zilizopo katika Magazeti ya Leo Jumatatu July 04, 2016  


Vibonzo:Katuni bora zaidi leo Jumatatu July 04, 2016 Bofya hapa 

LOWASSA APIGIWA SALUTI NA WANAJESHI LEO JUMAPILI JULY 03, 2016  Bofya hapa
CHADEMA Waapa Kutibua Mkutano wa CCM ,Vijana 2000 Kupelekwa Dodoma Kwa Ajili ya Kazi Hiyo Bofya hapa 

 Video:Chadema kuzuia Mkutano wa CCM wa kuchagua mwenyekiti wa chama Bofya hapa
Habari zilizopo katika Magazeti ya leo Jumapili July 03, 2016 Bofya hapa

Vibonzo: Katuni tano bora zaidi leo Jumapili July 03, 2016 Bofya hapa

TFF wajichanganya kwa Muro bofya hapa

Tamko la RC Makonda kuhusu mashoga waliopo jijini Dar es Salaam 


 Hatimaye TAKUKURU na TRA Wamtaja Mtu Aliyekuwa Akiibia Serikali Milioni 7 Kwa Kila Dakika Bofya hapa

 Ufafanuzi wa TRA kuhusu ongezeko la thamani kwenye huduma za kifedha Bofya hapa









Like page yetu ya facebook upate habari kwa urahisi na haraka zaidi BOFYA HAPA

Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top