News alert:Mtuhumiwa wa Ujambazi Maduka ya Pesa, Mauaji Msikitini Awatoroka Polisi

Taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza inaeleza kuwa mnamo tarehe 03.07.2016, majira ya 08:00 usiku katika maeneo ya Mlima wa Kiloleli Nyasaka wilaya ya Ilemela mkoa wa Mwanza, mtuhumiwa wa ujambazi katika maduka ya kutuma pesa kwa njia ya simu, pamoja na mauaji ya msikitini aliyejulikana kwa jina Hamisi Juma (38) mkazi wa Nyegezi aliyekuwa anashikiliwa na jeshi hilo, alitoroka ulinzi wa askari, wakati akiwapeleka askari wa upelelezi kuwaonyesha eneo lingine wanapojificha majambazi wenzake.

Aidha baada ya askari kufika kwenye eneo la tukio ghafla majambazi waliokuwa wamejificha katika mlima tajwa hapo juu walianza kurusha risasi kwa askari ndipo askari walipo taharuki na kuanza kujibu mashambulizi ya risasi kwa majambazi hao.

Pindi majibizano ya risasi yakiendelea kati ya watuhumiwa wa ujambazi ambao walikuwa wamejificha kwenye mlima, hali hiyo ilipelekea mtuhumiwa Bw. Hamisi Juma aliyekuwa chini ya ulinzi wa askari polisi kupata mwanya na kuwatoroka askari na kutokomea kusiko julikana.

Aidha a katika mapigano hayo askari walifanikiwa kukamata bunduki aina ya short gun ilyokatwa mtutu na kitako iliyokuwa na risasi moja chemba iliyotupwa na majambazi hao.

Hata hivyo taarifa hiyo imesema kuwa juhudi za kutafuta mtuhumiwa huyo zinaendelea na kuhakikisha anatiwa nguvuni na jeshi la polisi.

Katika tukio lingine la tarehe tajwa hapo juu majira ya saa 08:45 usiku katika eneo la Kiloleli, Kata ya Nyasaka Wilaya ya Ilemela, Mkoa wa Mwanza, mtuhumiwa wa ujambazi katika maduka ya kutuma na kupokea pesa kwa njia ya simu, pamoja na mauaji ya Msikiti wa Rahmani uliopo kata ya Mkolani aitwaye Mohamedi Bishof mwenye umri wa miaka 31, shombe wa Kiarabu mkazi wa Nyasaka aliruka kutoka ndani ya gari la polisi kwa nia ya kutaka kutoroka, lakini hata hivyo alianguka barabarani na kuumiakichwani na sehemu mbalimbali za mwili wake. Aidha mtuhumiwa huyo wa ujambazi alifariki dunia njiani wakati akipelekwa hospitali kupatiwa matibabu.

Taarifa ya jeshi hilo inasema kuwa wakati wa uhai wake marehemu alikiri kuwa ni kweli alihusika katika matukio ya mauaji naunyang’anyi wa kutumia silaha katika vibanda vya m-pesa, tigo pesa na airtel money.

Pindi marehemu anakamatwa alikutwa akiwa na electronic devices aliyokuwa akitumia kufanyia matukio ya uhalifu jijini Mwanza na nje ya Mwanza pamoja na kompyuta mpakato moja aina ya dell ambayo walikuwa wamepora katika tukio moja la unyang’anyi wa kutumia silaha kwenye tukio la tarehe 05.05.2016 katika eneo la Kishiri Center ambapo mwenye duka aliyejulikana kwa jina la Phares Gabriel alijeruhiwa na risasi kwenye mguu wa kulia na mkono wa kulia na kupora fedha ambazo hazijafahamika zilikuwa ni kiasi gani.

Majeruhi aliyepigwa risasi katika tukio hilo alipelekwa hospitali ya rufaa ya Bugando kupatiwa matibabu lakini baadaye alifariki dunia kutokana na majeraha ya risasi alizopigwa. Mwili wa marehemu mtuhumiwa upo Hospitali ya rufaa ya Bugando kwa uchunguzi na utambuzi.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza bado lipo katika jitihada kali za kuhakikisha watuhumiwa wote wanaodaiwa kuhusika katika uhalifu wanakamatwa na kufikishwakatika vyombo vya sheria.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Ahmed Msangi anawataka wananchi wa Jiji na Mkoa wa Mwanza kutulia huku wakiendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi, ili kuweza kufanya kazi vizuri na kufanikiwa kuwakamata wahalifu na silaha wanazotumia mapema na haraka iwezekanavyo.
Chanzo: EATV
HABARI KUU LEO BOFYA HAPA
















Like page yetu ya facebook upate habari kwa urahisi na haraka zaidi BOFYA HAPA

Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top