Takuma Asano wa Japan atua Arsenal




Takuma Asano ana umri wa miaka 21

Arsenal wamekubali kumsajili mshambulizi chipukizi kutoka Japan Takuma Asano.

Mshambulizi huyo mwenye umri wa
miaka 21 amejiunga na the Gunners akitokea klabu ya nyumbani ya Sanfrecce Hiroshima.

Kandarasi yake hata hivyo itakamilishwa baada ya kufanyiwa vipimo vya afya.

Arsenal imechapisha kwenye tovuti yake picha za mashambulizi huyo na kumkaribisha uwanjani emirati.

Takuma amewahi kuichezea Japan katika mechi 5 za kimataifa.

Takuma anatarajiwa kujumuishwa katika kikosi cha nchi hiyo kitakayoshiriki michezo ya Olimpiki mwezi ujao jijini Rio de Janeiro Brazil.

Takuma amecheza mechi 56 na kufunga mabao 11 katika ligi kuu ya Japan J-League.

Alishinda ligi hiyo ya J1 League mwaka wa 2013 na 2015, Japanese Super Cup 2013, 2014 na 2015,mwaka huo pia alituzwa kama chipukizi bora wa mwaka .

Kocha Arsène Wenger amemsifu mshambulizi huyo kwa ukakamavu wake

''Takuma ni mshambulizi machachari sana na bila shaka atatufaa zaidi katika siku za usoni.Bila shaka ameanza vyema taaluma yake na tunatazamia kukinoa zaidi kipaji chake kwa manufaa ya Arsenal''. 
HABARI KUU LEO BOFYA HAPA

LOWASSA APIGIWA SALUTI NA WANAJESHI LEO JUMAPILI JULY 03, 2016 Bofya hapa
CHADEMA Waapa Kutibua Mkutano wa CCM ,Vijana 2000 Kupelekwa Dodoma Kwa Ajili ya Kazi Hiyo Bofya hapa 

 Video:Chadema kuzuia Mkutano wa CCM wa kuchagua mwenyekiti wa chama Bofya hapa
Habari zilizopo katika Magazeti ya leo Jumapili July 03, 2016 Bofya hapa

Vibonzo: Katuni tano bora zaidi leo Jumapili July 03, 2016 Bofya hapa

TFF wajichanganya kwa Muro bofya hapa

Tamko la RC Makonda kuhusu mashoga waliopo jijini Dar es Salaam 


 Hatimaye TAKUKURU na TRA Wamtaja Mtu Aliyekuwa Akiibia Serikali Milioni 7 Kwa Kila Dakika Bofya hapa

 Ufafanuzi wa TRA kuhusu ongezeko la thamani kwenye huduma za kifedha Bofya hapa









Like page yetu ya facebook upate habari kwa urahisi na haraka zaidi BOFYA HAPA
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top