Mke wa Trump adaiwa kumuiga Michelle Obama

Melania awali alisifiwa sana kwa hotuba yake

Sherehe ya ufunguzi wa kongamano kuu la wajumbe wa chama cha Republican nchini Marekani imegubikwa na utata baada ya hotuba iliyotolewa na mke wa Donald Trump.

Hotuba hiyo ya Melania inadaiwa kuwa na maandishi yaliyotolewa kutoka kwenye hotuba ya mke wa Rais Barack Obama, Michelle, aliyoitoa miaka minane iliyopita.

Mke huyo wa Trump, ambaye ni mzaliwa wa Slovenia, amesema alipata usaidizi mdogo sana wakati wa kuandika hotuba hiyo, ambayo imesisitiza sana maadili ya kifamilia na kujumuishwa kwa watu wa matabaka yote.

Sehemu moja ya hotuba ya Bi Trump alisema: "Wazazi wangu walinifunza umuhimu wa kutia bidii kutafuta unachotaka maishani; kwamba neno lako ndilo linaweka uhusiano na unafaa kutenda unachosema na kutimiza ahadi; kwamba lazima uwaheshimu watu.”

Hotuba ya Bi Obama mwaka 2008 ilisema: "Mimi na Barack tulilelewa na maadili karibu sawa, kwamba unatia bidii kutafuta unachotaka maishani; kwamba neno lako linaweka uhusiano na kwamba unafaa kutenda unachosema utatenda; kwamba lazima uwaheshimu watu, hata kama huwafahamu, na hata kama haukubaliani nao.”


Maafisa wa kampeni wa Bw Trump hawajajibu madai hayo.
Wengi wa waliohutubu katika kongamano hilo linaloendelea mjini Cleveland, Ohio, wameangazia sana kutilia shaka uwezo wa mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton kuwa rais.

Meeya wa zamani wa New York Rudy Giuliani amewauliza wajumbe: “Nani anaweza kumwamini Bi Clinton amlinde?”

Awali, wajumbe wanaompinga Bw Trump waliandamana na kulalamika baada yao kuzuiwa kuwasilisha pingamizi zao.

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top