MASHABIKI WA ARSENAL WAMSHAMBULIA HENRY TWITTER


Nguli wa Arsenal Thierry Henry ameamua kuachana na kazi ya kufundisha timu ya vijana ya klabu hiyo baada ya kutofautiana na bosi wake Arsene Wenger na kuendelea kazi yake ya uchambuzi katika kituo cha runinga cha Sky Sports.

Kitendo cha kuondoka kwake kimezua malumbano makubwa sana miongoni mwa mashabiki wa Arsenal kwenye mitandao ya kijamii.
Henry aondoka Arsenal hii ndio sababu bofya hapa
Kwenye Tweet zake, Thierry Henry ameonekana kuelekeza lawama zote kwa Arsene Wenger.

Licha ya yeye mwenyewe kuamua kuchukua maamuzi hayo na kufanya kazi na Sky Sports na kuachana na Arsenal, Thierry Henry ameonekana kushusha lawama zote juu ya maamuzi hayo kwa Arsene Wenger.

Henry ameelezea kuondoka kwake kama “maamuzi ya Arsene Wenger”, kitu ambacho kinaashirikia kwamba wawili hao hawajaachana vizuri.

Tweet za Henry na majibu na namna alivyojibiwa




HABARI KUU LEO BOFYA HAPA






Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top