STARS YAPOROMOKA VIWANGO VYA FIFA, UGANDA VINARA CECAFA

Shirikisho la soka Duniani, FIFA limetoa orodha ya viwango vya ubora kwa mataifa mbalimbali duniani kwa mwezi Septemba.

Orodha inaonesha kwamba, Tanzania imeporomoka kwa nafasi nne kutoka 124 hadi kushika nafasi ya 132.

Kufungwa dhidi ya Nigeria katika mchezo uliokuwa wa kusaka tiketi ya kufuzu Afcon mwaka 2017 pengine ndiyo sababu kubwa ya Tanzania kuporomoka.

Uganda bado wameendelea kuwa bora Afrika Mashariki na ukanda wote wa CECAFA kwa ujumla wakishika nafasi ya 65 duniani na 15 barani Afrika.

Rwanda wanafuata kwa karibu baada ya kupanda mpaka nafasi ya 107 kutoka nafasi ya 121.

Barani Afrika, Ivory Coast wameendelea kuwa kileleni, huku wakishika nafasi ya 34 duniani, wakifuatiwa na Waarabu wa Algeria, Senegal na Ghana.

Kinara wa ulimwengu wanabaki kuwa Argentina wakfuatiwa kwa karibu na Ubelgiji, Ujerumani, Colombia na Brazil.

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top