Profesa Mkilaha wa UDSM afariki kwa kujipiga risasi




Profesa Mkilaha, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 
Kwa ufupi

Dar es Salaam. Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Idd Mkilaha, inadaiwa amefariki dunia jioni hii nyumbani kwake
Tegeta, Dar es Salaam baada ya kujipiga risasi.


Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro, amesema polisi wanaendelea kuchunguza sababu zilizosababisha tukio hilo.


“Ni kweli tukio hilo limetokea, amekufa kwa kujipiga risasi, lakini tunachunguza kubaini kama ilikuwa ni bahati mbaya au alidhamiria kufanya hivyo,” amesema Sirro.


Hata hivyo, amesema taarifa zaidi atazitoa kesho.


Profesa Mkilaha alikuwa pia Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra).

Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top