Arsene Wenger anaamini Arsenal watakamilisha usajili wa beki wa Valencia Shkodran Mustafi kabla ya dirisha kufungwa rasmi.
Kwa muda mrefu Arsenal wamekuwa wakihusishwa na usajili wa beki huyo wa Kijerumani lakini dili hilo bado linaonekana kusuasua, hali iliyopelekea hali ya sintofahamu kwa mashabiki wa klabu hiyo kutokana na ukosefu wa usajili wa maana kwenye timu hiyo.
Wenger amesisitiza bado maridhiano yanaendelea kati ya pande mbili lakini hakusita kuonesha kufedheheshwa na ukosefu wa wachezaji aliowahitaji.
“Mustafi? Naamini tutakamilisha hilo suala,” alisema Wenger. “Bado tunapambana kuhakikisha tunapata wachezaji tunaowahitaji.
“Ni moja ya wachezaji tunaowahitaji kwa kiasi kikubwa. Bado tunaendelea na maridhiano.”
Wakuu Wa Shule Za Msingi 68 Kuvuliwa Vyeo Vyao Jijini Dar Es Salaam bofya hapa
Ajira zaidi bofya hapa
Azam Mabingwa Ngao ya Jamii bofya hapa
Post a Comment
Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)