Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemthibitisha Bw. Gerson Partinus Msigwa kuwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Rais, (Director of Presidential Communication - DPC).
Taarifa iliyotolewa leo Jumatano Agosti 31,2016 na Katibu Mkuu Ikulu Bw. Peter Ilomo imeeleza kuwa Bw. Gerson Partinus Msigwa amethibitishwa kuanzia leo tarehe 31 Agosti, 2016 kushika wadhifa huo.
Kabla ya uthibitisho huo, Bw. Gerson Partinus Msigwa alikuwa Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Rais, katika Ofisi ya Rais Ikulu kuanzia tarehe 17 Novemba, 2015.
Jaffar Haniu
Kaimu Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi.
Dar es Salaam
31 Agosti, 2016
Nafasi zaidi za kazi bofya hapa
Ufafanuzi wa CHADEMA kuhusu taarifa ya kuahirishwa Operesheni UKUTA. bofya hapa
Profesa Lupumba,Magdalena Sakaya na Abdul Kambaya Wavuliwa Uanachama CUF Bofya hgapa
Ufafanuzi wa CHADEMA kuhusu taarifa ya kuahirishwa Operesheni UKUTA. bofya hapa
Profesa Lupumba,Magdalena Sakaya na Abdul Kambaya Wavuliwa Uanachama CUF Bofya hgapa
Post a Comment
Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)