ALIYEKUWA rais wa pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kati ya
tarehe 7 Aprili 1972 hadi 30 Januari 1984, Aboud Jumbe Mwinyi amefariki
dunia mchana wa leo nyumbani kwake Kigamboni, jijini Dar es Saalam
baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Kifo cha mwanasiasa huyo mkongwe kimethibitishwa na mmoja wa wanafamilia ya marehemu.
baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Kifo cha mwanasiasa huyo mkongwe kimethibitishwa na mmoja wa wanafamilia ya marehemu.
Marehemu Jumbe atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa wa kuiongoza
serikali ya mapinduzi ya Zanzibar akichukua nafasi ya aliyekuwa rais wa
nchi hiyo marehemu Abeid Aman Karume aliyefariki mwaka 1972.
(Ujumbe wa Zitto Kabwe kufuatia kifo Rais Mstaafu wa Zanzibar bofya hapa)
Enzi za uhai wake akiwa rais wa serikali ya mapinduzi Zanzibar alishirikiana na rais wa wakati huo wa Tanzania na mwenyekiti wa chama cha TANU marehemu Julius Nyerere kuanzisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuvunja vyama vya TANU na ASP na kuunda chama kimoja cha CCM.
(Ujumbe wa Zitto Kabwe kufuatia kifo Rais Mstaafu wa Zanzibar bofya hapa)
Enzi za uhai wake akiwa rais wa serikali ya mapinduzi Zanzibar alishirikiana na rais wa wakati huo wa Tanzania na mwenyekiti wa chama cha TANU marehemu Julius Nyerere kuanzisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuvunja vyama vya TANU na ASP na kuunda chama kimoja cha CCM.
Post a Comment
Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)