Bintiye Obama afanya kazi mgahawani

Sasha Obama, 15, akifanya kazi
Sasha Obama, 15, akifanya kazi

Sasha Obama, bintiye Rais wa Marekani Barack Obama, ameamua kuacha 'starehe' za ikulu ya White House na kuanza kufanya kazi katika mgahawa mmoja, vyombo vya habari nchini Marekani vinaripoti.

Binti huyo wa umri wa miaka 15 ameanza kufanya kazi ya kuwahudumia wateja katika mgahawa mmoja ulioko Martha's Vineyard, Massachusetts.

Sasha, ambaye anatumia jina lake kamili, Natasha, aliandamana na maafisa sita wa ulinzi wa secret service siku yake ya kwanza kazini, gazeti la Boston Herald linaripoti.

Familia ya Obama hutembelea eneo hilo sana wakati wa likizo.

Picha zinazosambazwa zinamuonesha bintiye huyo mdogo wa Obama akiwa amevalia sare ya hoteli akifanya kazi.

Mfanyakazi mmoja katika mgahawa huo aliambia gazeti hilo la Herald: "Tulikuwa tunashangaa ni kwa nini kulikuwa na watu sita walikuwa wanamsaidia msichana huyu, lakini baadaye tukagundua alikuwa nani."
 
Ajira Zaidi bofya hapa


 

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top