Polisi Warudisha Vifaa vya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Vilivyokuwa Vinashikiliwa Tangu Mwaka Jana Baada ya Uchaguzi

Baada ya vifaa vyao vya ofisi zikiwamo kompyuta 25 kushikiliwa na polisi kwa miezi 10, hatimaye jana Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wamerejeshewa.
Oktoba mwaka jana, polisi walikwenda katika tawi la ofisi ya LHRC Kawe, kisha kuchukua kompyuta za mezani 24 na mpakato tatu huku wakiwashikilia waangalizi 25 wa uchaguzi, kwa kile ilichodai kituo hicho kilikuwa kinakusanya na kusambaza taarifa za matokeo ya urais yasiyo rasmi.


Mkurugenzi wa kituo hicho, Dk Hellen Kijo-Bisimba alithibitishia kupata vifaa hivyo vilivyokuwa vikishikiliwa na Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.


Dk Bisimba alisema wiki iliyopita waliwapigia simu polisi kuwaomba kurejeshewa vifaa hivyo, zikiwamo simu 25.


“Jana (juzi) polisi walitupigia simu.Leo (jana) tumekwenda kuchukua mali zetu na zote zipo kamili isipokuwa kuna kompyuta moja haifanyika kazi,” alisema.


Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Simon Sirro alipopigiwa simu yake ilipokewa na msaidizi wake na kudai yupo mkutanoni.

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top