Leicester yamsajili mshambuliaji wa Nigeria




Ahmed Musa

Klabu ya Leicester City imemsajili mshambuliaji wa Nigeria Ahmed Musa kutoka CSKA Moscow kwa kandarasi ya miaka 4 itakayogharimu pauni milioni 16.

Southampton,Everton na West Ham walikuwa wakitafuta saini ya mchezaji huyo.

Musa ni mchezaji wa nne kusajiliwa na Leicester baada ya kipa Ron-Robert Zieler ,beki Luis Hernandez na kiungo wa kati Nampalys Mendy.

Mchezaji huyo alijiunga na CSKA mwaka 2012 na kufunga mabao 54 kati ya mechi 168 alizocheza,na amefunga mabao 11 katika mechi 58 alizochezea Nigeria tangu aanze kucheza mwaka 2010.

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top