Ronaldo amaliza msimu na rekodi ya dunia


Licha ya Real Madrid kushindwa kutwaa kombe la Ligi Kuu y Hispania (La Liga) lakini hilo halijamzuia staa wa klabu hiyo, Cristiano Ronaldo kumaliza msimu na rekodi ambayo haijawahi kuwekwa awali.

Katika mchezo wa mwisho wa La Liga ambao Real Madrid iliibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Deportivo la Coruna na Ronaldo kufunga magoli mawili ambayo yamemwezesha kuweka rekodi ya dunia.

Magoli hayo yalikuwa ya 35 kwa La Liga msimu huu na katika michuano ya Ulaya amefunga magoli 16 hivyo kuweza kufikisha magoli 51.

Rekodi hiyo ni kufunga magoli zaidi ya 50 kwa misimu sita mfulizo, rekodi ambayo hapo awali hhaijawahi kuwekwa na mchezaji yoyote katika historia ya soka.

Kwa kipindi chote ambacho Ronaldo amechezea Real Madrid ameifungia klabu hiyo magoli 364 katika michezo 347.

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top