Leo Rais Magufuli amefungua rasmi awamu ya kwanza ya miundombinu na utoaji wa huduma ya usafiri wa haraka wa mabasi (BRT) katika
Jiji la Dar es Salaam.
Akizungumza kabla ya kufungua rasmi awamu ya kwanza ya mradi huo Rais Magufuli ameiomba Benki ya Dunia kuharakisha mchakato wa kutoa fedha za mkopo utakaowezesha kuanza kwa ujenzi wa barabara za juu katika makutano ya barabara ya Ubungo (Ubungo Interchange) ili kuongeza ufanisi wa mradi.
Pia ametoa onyo kali kwa magari ya kawaida, bajaji na pikipiki kuingia katika barabara za mabasi ya mwendo kasi huku akisisitiza msimamo wake wa kutaka yatolewe matairi pindi yanapokamatwa
==> Isikilize hotuba yake hapo chini
Post a Comment
Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)