Trump Kaanza Kuwatimua Watu Marekani, Tayari Wasomali 90 na Wakenya 2 wameondolewa Marekani


Raia takriban 90 wa Somalia na wawili wa Kenya wametimuliwa kutoka Marekani saa chache baada ya taarifa kuibuka kwamba Rais Donald Trump atakabiliana na watu wanaoishi nchini humo kinyume cha sheria.


Wote wamewasili katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi.


Msemaji wa serikali ya Kenya Eric Kiraithe ameambia BBC kwamba raia hao wa Somalia watasafirishwa moja kwa moja hadi Mogadishu.


Bw Trump alisema Jumatano itakuwa siku muhimu kwa usalama wa Marekani.


Anatarajiwa kuweka masharti makali kwa raia wa mataifa saba ya Mashariki ya Kati na Afrika yenye idadi kubwa ya Waislamu wanaotafuta viza za kwenda Marekani.


Nchi hizo ni Syria, Iraq, Iran, Libya, Somalia, Sudan na Yemen

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top