Waziri Simbachawene atoa agizo jipya kwa machinga



Waziri wa TAMISEMI George Simbachawene amewataka wamachinga kutotafsiri vibaya agizo la Rais Magufuli kuwa halikumaanisha wafanye biashara kiholela mahala popote bila utaratibu bali wazingatie sheria zilizopo zikiwamo za mipango miji na usafi.


Simbachawene pia amewaagiza wakuu wa mikoa na wilaya pamoja na mamlaka za serikali za mitaa, kuhakikisha wanatekeleza agizo la Rais John Magufuli la kuwatafutia maeneo ya kufanyia biashara wafanyabiashara hao na kuwashirikisha kwenye mchakato mzima wa kubaini maeneo yenye wateja na miundombinu rafiki.


Aidha, watendaji nao wametakiwa kutotumia tafsiri hiyo kususa na kuwaacha wamachinga wafanye biashara zao kiholela.


Amesema endapo utaratibu huo utafuatwa pamoja na mambo mengine utaweza kurasimisha shughuli za wamachinga hali itakayosaidia pia kundi hilo kuchangia mapato ya halmashauri kwa kiasi kikubwa na kuondoa kabisa tabia ya kufukuzana fukuzana kila kukicha.

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top