Facebook kukabiliana na akaunti feki

Mwanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg amekuwa akipambana kudhibiti habari za uongo kwa miezi ya hivi karibuni

Mwanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg amekuwa akipambana kudhibiti habari za uongo kwa miezi ya hivi karibuni

Mtandao wa Facebook umesema umeanzisha upelelezi kukabiliana na akaunti feki za watumiaji.

Tiyari umeshaanza kutumia wafanyakazi kutoka nje ya kampuni hiyo watakaoweza kugundua kompyuta zinazotumika mara kwa mara ambazo zinahusiana na akaunti hizo.

Facebook wamekuwa wakilalamikiwa kwa kushindwa kuchukua hatua juu ya wale wanaoghushi habari kwa kutumia akaunti hizo ikiwemo mtu mmoja aliyewahi kudanganya kuwepo kwa mwizi aliyekuwa na silaha ya moto katika mgahawa mmoja mjini Washington taarifa ambazo hazikuwa na ukweli wowote.

Inasemekana kuwa baadhi ya watu hutumia pia akaunti feki kuweka habari kwenye facebook ili wapate watizamaji wengi na hivyo kuongeza fedha.

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top