Katumbi asema atarejea DR Congo kuwania urais

Bw Katumbi amekuwa akiishi Ubelgiji

Mwanasiasa aliyetangaza nia ya kuwania urais nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Moise Katumbi, ambaye amekuwa akiishi uhamishoni, amesema atarejea nyumbani.

Bw Katumbi, rafiki wa karibu wa zamani wa Rais Joseph Kabila amekuwa akiishi Ubelgiji.

Aliondoka nchini DR Congo mapema mwaka huu baada ya kutuhumiwa kuajiri mamluki kwa lengo la kupindua serikali ya Rais Kabila.

Na baadaye mwezi Juni, alipatikana na hatia ya kuuza nyumba kinyume cha sheria na akahukumiwa kifungo cha miezi 36 jela.

Akiongea na BBC akiwa ziarani London, Bw Katumbi amesema:

"Mimi ni raia wa Congo, nitarejea nyumbani na bado nawania urais. Tuhuma kwamba nilipanga kupindua serikali zinakusudiwa kunizuia."

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top