Hatimaye Wasichana wa Chibok waungana na familia zao



 Wasichana wa Chibok, Nigeria

Wasichana wa shule 21 ambao walitekwa na wapiganaji wa kiislamu katika mji wa Chibok hatimaye wameungana tena na familia zao.

Wasichana hao waliokuwa wakishikiliwa kwa takriban miaka miwili na wapiganaji wa Boko Haram wamesimulia mateso waliyopitia.

Mmoja wa wasichana hao anasema alidhani kuwa siku ya kuachiwa kwake haitakuja kutokea. Huku mzazi mmoja wapo akisema kwamba wanaendelea kuwaombea dua wasichana ambao bado wanashikiliwa.

Msemji wa Rais wa Nigeria Garba Shehu ameliambia Shirika la Habari la Reuters wapiganaji ambao waliwaachia wasichana hao siku ya Alhamisi bado wanawashikilia wasichana wengine wapatao 83.

Zaidi ya wanafunzi 250 kutoka Chobok walikamatwa mateka April 2014.
 

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top