Heka heka za usajili barani ulaya




Heka heka za vilabu mbalimbali barani ulaya kuimarisha vikosi vyao zimendelea kwa kusajili nyota wapya watakaozichezea timu hizo.

Klabu ya Norwich City imekamilisha usajili golikipa Michael McGovern raia wa Ireland ya kaskazini akitokea timu ya Hamilton ya Scotland kwa mkataba wa mitatu.

Nayo timu ya Burnley imewasajili winga Johann Berg Gudmundsson na golikipa Nick Pope kutoka Charlton Athletic. Wote wawili wamesajiliwa kwa mkataba wa miaka mitatu huku dau la usajili likiwa halikuwekwa wazi.

Beki wa Wales Jazz Richards amesaini mkataba wa miaka mitatu kuitumikia Cardiff City akitokea Fulham.
 
 

 

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top