Naibu waziri Tamisemi,Suleiman Jafo anusurika kifo ajalini Mbeya


Naibu Waziri wa Tamisemi, Suleiman Jafo amepata ajali eneo la Katela Kata ya Kiwira, Wilaya ya Rungwe Mbeya.


Ajali hiyo imehusisha gari dogo aina ta Corola iliyokuwa ikotokea Mbeya kwenda Rungwe na Naibu Waziri Selemani Jafo alikuwa akitokea Tukuyu kikazi.


Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Mariam Mtunguja amesema katika gari laWaziri walikuwa watatu, Waziri Jafo mwenyewe Katibu wake na Dereva na wote walitoka salama katika ajali hiyo.


Alisema baada ya kupata ajali  walipelekwa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya ambapo walifanya uchunguzi kubaini kama wameumia  au laa! Lakini bahati nzuri Daktari aliyewafanya uchunguzi alisema hawakuumia


Alisema baada ya hapo Waziri na wenzake waliendelea na safari yao kuelekea mjini Dodoma kwa ajili ya kuwahi vikao vya Bunge
Gari lililoigonga gari la Naibu Waziri likiwa limetupwa korongoni.
Askari wa usalama barabaran wilayani Rungwe, Mbeya wakipima ajali ilivyotokea
Picha zote kwa hisani ya Mbeya yetu
 
 

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top