
.
Iliwachukua dakika 15 tu Liverpool kupata bao la kwanza kupitia kwa Divock Origi baada ya kuusindikiza mpira wavuni, kabla ya Roberto Firmino kuongeza lingine baada ya kuunganisha krosi nzuri iliyochongwa na Nathaniel Clyne na kufanya matokeo kuwa 2-0.
Origi alitaka tena kuongeza lingine baadaye lakini mpira uliokolewa na kipa wa Burton Albion Stephen Bywater.
Tom Naylor alijifunga mwenyewe na kuipatia Liverpool bao la tatu dakika ya 61, kabla ya Daniel Sturridge ambaye aliingia kutokea benchi kufunga mawili mnamo dakika ya 78 na 83 na kuhitimisha karamu ya mabao 5-0 kwa Liverpool.
Post a Comment
Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)