Tundu Lissu afikishwa tena Mahakamani

HATIMAYE Jeshi la Polisi Jijini Dar es salaam limemfikisha rasmi kizimbani Mwanasheria Mkuu wa Chadema ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo Singida Mashariki wilaya ya Ikungi mkoani Singida.
Tundu Lissu ambaye alikamatwa Juzi mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wa hadhara Ikungi, Singida na kusafirishwa usiku, kulazwa Chamwino Dodoma na kufikishwa Dar jana saa saba mchana alilazwa rumande kabla ya kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mchana wa leo.


Akionekana mwenye kujiamini, Lissu amewasili Mahakamani Kisutu akitokea mahabusu ya Kituo kikuu cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam saa nane na dakika arobaini na nane (14:48) akiwa kwenye gari yenye namba za usajili T 517 BET Corolla na akisindikizwa na ulinzi mkali wa jeshi la polisi.



Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top