Mourinho: Wenger na Klopp hawana ''maadili''

Mkufunzi Jose Mourinho
Mkufunzi Jose Mourinho

Mkufunzi wa klabu ya Manchester United Jose Mourinho anasema kuwa ukosoaji uliotolewa na kocha wa Arsenal Arsene Wenger na mwenzake wa Liverpool Jurgen Klopp ''hauna maadili''.

Wenger na Klopp wamelalamikia uhamisho wa pauni milioni 100 wa Paul Pogba.

''Kuna vitu ambavyo nikifanya havina maadili,lakini wengine wakifanya ni jambo la kawaida'',alisema Mourinho.

Mkufunzi huyo wa United ameongezea kuwa atamsajili mchezaji mzuri wa kiungo cha kati katika siku chache zijazo na Pogba ni muhimu.

''Kwa sasa tuna wachezaji 22,alisema.Tutakuwa na 23.Ni mchezaji wa Juve hadi pale atakapokuwa rasmi nje''.Soko la uhamisho linafungwa tarehe 31 mwezi Agosti.

''Tunajaribu kila tuwezalo kufunga soko letu la ununuzi kwa haraka iwezekanavyo''.
 

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top