Mshabuliaji Carlos Bacca amefunga hat-trick kwenye mechi ya kwanza ya AC Milan katika ufunguzi wa msimu mpya wa Serie A dhidi ya Torino.
Nyota huyo mwenye miaka 29 aliyehusishwa kujiunga na West Ham, aliifungia Milan bao la kwanza kwa kichwa kabla ya mapumziko kabla ya Andrea Belotti kusawazisha.
Bacca akafunga bao jingine kisha kumalizia hat-trick yake ya kwanza ndani ya Serie A kwa mkwaju wa penati.
Daniele Baselli akaifungia Torino bao dakika za majeruhi dakika chache kabla ya golikipa wa Ac Milan Gianluigi Donnarumma kupangua penati ya Belotti dakika za lala salama baada ya Gabriel Paletta kuzawadiwa kadi nyekundu kutokana na mchezo mbaya.
Wakuu Wa Shule Za Msingi 68 Kuvuliwa Vyeo Vyao Jijini Dar Es Salaam bofya hapa
Ajira zaidi bofya hapa
Azam Mabingwa Ngao ya Jamii bofya hapa
Post a Comment
Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)