Guardiola na Man City wachapwa na Bayern

Manchester City watakutana na Manchester United Jumatatu

Manchester City, wakicheza mechi yao ya kwanza ya kujiandaa kwa msimu mpya chini ya meneja mpya Pep Guardiola, wamechapwa bao moja kwa bila na klabu ya zamani ya meneja huyo Bayern Munich.

City walifungwa bao moja na Erdal Ozturk wa Bayern, ambao kwa sasa mkufunzi wao ni Carlo Ancelotti.

Wachezaji wengi nyota hawakucheza mechi hiyo kwani bado wanapumzika baada ya kushiriki Euro 2016 na Copa America.

Guardiola alichezesha wachezaji 12 wa timu ya vijana, mechi hiyo iliyochezewa Allianz Arena.

Mlinda lango wao alikuwa Angus Gunn, mwanawe mchezaji nyota wa zamani wa Norwich Bryan.

City sasa wataelekea Uchina ambapo watacheza dhidi ya Manchester United siku ya Jumatatu.

Watasafiri na Sergio Aguero, David Silva, Nolito, Raheem Sterling na Joe Hart.
Kikosi cha Manchester City kipindi cha kwanza:

Caballero, Maffeo, Adarabioyo, Kolarov, Angelino, Fernando, Fernandinho, Zinchenko, Barker, Iheanacho, Navas
Kipindi cha pili:

Gunn, Maffeo, Adarabioyo, Kolarov, Angelino, Clichy, Fernando, Fernandinho, Delph, Bony, Navas

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top