Serikali Yakanusha Madai Kuwa Haina Mpango wa Kuwapanga Vijana Waliohitimu Kidato cha Nne kwenda kidato cha Tano


Serikali imekanusha madai ya kuwepo kwa taarifa ya kuwa haina mpango wa kuwapanga vijana waliohitimu kidato cha nne kwenda kidato cha tano kwa sababu mbalimbali.


Akiongea leo Bungeni Mjini Dodoma, Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amesema kuwa taarifa hizo ni za uvumi na serikali kwa sasa ipo katika mchakato wa upangaji wa majina hayo na wakati wowote mwisho mwa mwezi majina yatakuwa yametolewa.


Waziri Mkuu Majaliwa amesema moja ya sababu za kuchelewa kwa matokeo hayo ni pamoja na wizara kubadili mfumo wa GPA, kwenda Division hivyo mchakato huo ndio unafanywa na serikali ili wanafunzi wote wapate madaraja yao na waweze kupangiwa shule.


Mhe. Majaliwa amesema suala la upangaji halikuwa kwa kidato cha tano peke yake bali pia wale wanaokwenda vyuo mbalimbali na kusema kuwa baada ya kukamilika watatoa majibu yao wiki mbili kabla ili wazazi waweze kujiandaa kuwapeleka watoto mashuleni.
 


Habari zilizopo katika Magazeti ya Leo Alhamisi June 23, 2016 Bofya hapa
Vibonzo:Katuni Tano bora zaidi leo Alhamisi June 23, 2016 Bofya hapa

Like page yetu ya facebook upate habari kwa urahisi na haraka zaidi BOFYA HAPA

HABARI KUU LEO BOFYA HAPA
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top