Serikali Yafuta Utaratibu Ilioupendekeza Kwa Taasisi Za Dini Kulipa Kodi Kwanza Kwa Bidhaa Watakazonunua


Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Phillip mpango amesema amefuta utaratibu alioupendekeza bungeni wa taasisi za dini kulazimika kulipa kodi kwanza kwa bidhaa watakazonunua au kuagiza nje na kodi hiyo

kurejeshwa baada ya ukaguzi kufanyika.


Waziri Mpango ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari alipokuwa akitoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja za wabunge kuhusu Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017.


Amesema kwa kutambua mchango mkubwa wa taasisi mbalimbali za kidini katika utoaji huduma za elimu na afya anapendekeza kufuta utaratibu huo na badala yake Serikali itaimarisha zaidi hatua mbalimbali za udhibiti wa msamaha ya kodi.
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top