Mtoto Anajisiwa na Kisha Kuuawa Kwa Kunyongwa

Eneo la Unga Limited, jijini Arusha
Mtoto wa miaka minne amenajisiwa na kuvunjwa shingo na kutupwa kandokando ya njia ya watembea kwa miguu karibu na mfereji wa maji umbali wa mita 50 kutoka nyumbani kwao jijini Arusha.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Yusuf Ilembo, tukio la kunajisiwa kwa mtoto huyo wa kike lilitokea Juni 20, mwaka huu saa 3.30 usiku kwenye makaburi ya baniani Kata ya Unga Limited.


Kaimu Kamanda wa Polisi Ilembo alidai mtoto huyo ambaye kwa sasa ni marehemu alikuwa akicheza na wenzake nje kidogo ya nyumbani kwao na ilipofika saa 12 jioni kwa mujibu wa marafiki zake (majina yamehifadhiwa) wanasema alifika mtu mmoja mwanamume mrefu.


Kwa mujibu wa watoto hao, mwanamume huyo alikuwa amevaa suruali na kumwambia mtoto huyo amfuate akamnunulie pipi na hapo ndipo alipomfuata huyo mwanamume huyo na hakurudi tena.


Habari zilizopo katika Magazeti ya Leo Alhamisi June 23, 2016 Bofya hapa
Vibonzo:Katuni Tano bora zaidi leo Alhamisi June 23, 2016 Bofya hapa

Like page yetu ya facebook upate habari kwa urahisi na haraka zaidi BOFYA HAPA

HABARI KUU LEO BOFYA HAPA
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top