Mlipuko wakumba hoteli mjini Mogadishu

 
 Wanajeshi wa Amisson nchini Somalia

Mlipuko mkubwa umekumba hoteli moja katikati ya mji mkuu wa Somalia Mogadishu na kuna sauti za ufyatulianaji wa risasi katika kile kinachoaminika huenda ni shambulio la wapiganaji wa al-Shabab.

Kulingana na mwandishi wa BBC Ibrahim Aden mjini Mogadishu, mlipuko huo ulikumba hoteli ya Naso Hablod ikiwa ni hatua chache kutoka kwa uwanja wa ndegewa mji huo.

Hakuna ripoti zozote za majeruhi.

Ripoti zinasema kuwa huenda kulikuwa na mlipuko wa pili. Shambulio Somalia

Wapiganaji wa al-Shabab hutekeleza mashambulio ya mara kwa mara katika mji huo kwa lengo la kuiangusha serikali inayoungwa mkono na mataifa ya magharibi.

''Walianza na mlipuaji wa kujitolea muhanga na baadaye kuvamia.Kwa sasa wako ndani na ufyatuliaji mkubwa wa risasi unaendelea'' ,alisema msemaji wa polisi meja Nur Farah.
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top