Aliyetishia kumuua Trump mitandaoni aonja joto la jiwe

Maafisa Usalama wa Rais mteule wa Marekani, Donald Trump wamemtembelea mtu mmoja aliyetishia kumuua kiongozi huyo kwa ujumbe alioweka kwenye mitandao ya kijamii.


Vyanzo vya vyombo vya dola viliuambia mtandao wa TMZ kuwa kikosi maalum cha mashushu wa usalama cha Trump pamoja na Mkuu wa Polisi msaidizi wa Ohio, Jumatatu ya wiki hii walifika nyumbani kwa mtuhumiwa huyo aliyeweka ujumbe wake kwenye mitandao Novemba 14 mwaka huu, ukisoma “Kill Trump” (Muue Trump).


Ilielezwa kuwa kikao kati ya maafisa hao wa usalama nyumbani kwa mtu huyo anayetumia jina la ‘Micah’, kilienda vizuri ambapo aliwaeleza kuwa alikuwa anatania tu huku akisisitza kuwa huenda akapata wazo hilo pale ambapo Trump ataanza kutekeleza ahadi zake tata.


Micah pia alithibitisha kutembelewa na maafisa hao wa usalama na kueleza kuwa waliridhika na maelezo yake kuwa alikuwa anafanya utani tu, hivyo waliondoka.


Trump amekuwa akipata vitisho vya kushambuliwa tangu alipokuwa akiendesha kampeni zake. Mara kadhaa maafisa usalama walimuondoa ghafla jukwaani baada ya kuhisi jaribio la kutaka kumdhuru kutoka kwa wahudhuriaji.

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top