Trump azua mjadala tena Marekani



Trump amesema Clinton atafuta haki ya raia kumiliki silaha

Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani, Donald Trump, amezua mjadala mpya baada ya kuwahimiza wafuasi wake wenye bunduki kumzuia mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton, kubatilisha haki yao ya kikatiba ya kumiliki silaha.

Bw Trump alikuwa akihutubu katika mkutano wa siasa katika jimbo la North Carolina.

Bw Trump alikuwa amesema kwamba iwapo Bi Clinton atashinda basi atateua majaji wa Mahakama ya Juu ambao watafanikisha kuondolewa kwa haki ya raia kumiliki bunduki.

Alidokeza kwamba ni hatua ya raia pekee, ambayo inaweza kuzuia hilo lisifanyike.

Maafisa wa kampeni wa Clinton wameshutumu matamshi ya Trump na kusema ni hatari.

Lakini washauri wake wamesema alikuwa tu anawahimiza watu wanaoamini katika haki ya raia kumiliki silaha watumie kura zao kufanya uamuzi.
 

 

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top