Mwigulu Nchemba Awaonya Polisi Wanaowabambikiza Kesi Raia



Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba amewaambia askari wa jeshi la Polisi mkoani Katavi kufanya kazi kwa taratibu na sheria bila kumuonea mtu yeyote hasa wanyonge
.

Waziri Mwigulu ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya kutembelea makazi ya watanzania wapya pamoja na kuzungumza na askari wa jeshi la polisi, Magereza pamoja na Uhamiaji.


Mhe. Mwigulu amesema kuwa Askari hao waondokane na tabia ya matukio ya kuwabambikizia kesi raia kwa maslahi binafsi na kuwaonea na kusema kuwa serikali kali ya awamu ya tano haitamfumbia macho askari atakayebainika kufanya hivyo.


Aidha Waziri Mwigulu amechukua fursa hiyo kuwapa hamasa Askari hao kwa kusema kuwa serikali itawaboreshea maslahi yao kadri bajeti itakavyoruhusu ili waweze kufanya kazi kwa weledi zaidi.


Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top