Picha: Mshindi wa shindano la Miss World 2016 lililofanyika jana Marekani


Jana, Jumapili Disemba 18, 2016 jijini Washington DC, Marekani lilifanyika shindano kubwa la kumsaka Mrembo wa Dunia (Miss World 2016) ambapo nchi mbalimbali zilishiriki kwa kuwapeleka warembo walioibuka na ushindi katika nchi hizo.

Shindano hilo lilimalizika kwa Mrembo kutoka nchini Puerto Rico, Stephanie Del Valle (19) kunyakuwa taji la Mrembo wa Dunia 2016 (Miss World 2016).


Mrembo huyo alitangazwa mshindi baada ya kuwashinda warembo wengine kutoka nchi 116 duniani kote na Tanzania ikiwa moja wapo.


Mshindi wa pili ni Yaritza Miguelina Reyes Ramirez kutoka Jamhuri ya Dominican huku nafasi ya tatu ikiwenda kwa Natasha Mannuela kutoka Indonesia.


Hapa chini ni picha za tukio hilo lililofanyika jana.








Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top