MSHAMBULIAJI wa Yanga, Amis Tambwe amesema siri ya kuendelea kutikisa nyavu katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara bila kushuka, ni kwa vile amekuwa hasikilizi maneno ya mashabiki uwanjani.
Alisema mchezaji yeyote kama anahitaji kufanikiwa na kufanya vizuri katika ligi hiyo hapa nchini hana budi kuziba masikio ya mashabiki na kufanya kile ambacho kimemleta katika timu vinginevyo ni rahisi kupotea.
Tambwe hivi karibuni aliifungia bao timu yake katika mchezo dhidi ya Simba, ingawa inadaiwa kabla ya kufunga aliushika kwa mkono mpira huo.
Akizungumza na gazeti hili, mchezaji huyo wa zamani wa Simba, alisema anawajua mashabiki wengi wa soka wamekuwa ni wazungumzaji, na kwamba kama angekuwa anawafuatisha angekuwa ameshuka kiwango.
“Siku zote ukitaka kufanikiwa katika Ligi ya Tanzania ni lazima upambane kweli na kuacha kusikiliza maneno ya mashabiki, kwani ukiwafuatisha utaanguka na kupotea kabisa,” alisema.
Tambwe tangu kujiunga na Simba msimu wa mwaka 2013 na msimu uliopita Yanga, amekuwa akizidi kuonesha ubora wake katika kufumania nyavu huku msimu uliopita akiibuka kuwa mfungaji bora.
Alisema amejipanga kuhakikisha anaendelea kufanya vizuri sio katika kuifunga Simba bali katika michezo yote.
PICHA 5: Tingatinga Lilivyofukua mamilioni yaliyokuwa Yamefichwa ardhini bofya hapa
Waziri atolea maelezo taarifa ya serikali kuhakiki watumishi wanavyotumia mishahara yao bofya hapa
Waziri atolea maelezo taarifa ya serikali kuhakiki watumishi wanavyotumia mishahara yao bofya hapa
TCRA yakipa onyo kali kituo cha runinga cha Clouds, Yakifungia kwa miezi 3 kipindi cha 'Take One' kwa kukiuka kanuni za utangazaji. bofya hapa
Polisi Aliyerekodiwa Akipokea Rushwa Kuchukuliwa Hatua bofya hapa
Jeshi La Polisi Nchini Latoa Onyo Kali Kwa Wananchi Wanaojichukulia Sheria Mkononi. bofya hapa
Tanzania na Congo DRC zimesaini mkataba wa makubaliano kutafuta mafuta Ziwa Tanganyika bofya hapa
Mambo Muhimu Waliyoyajadili Rais Magufuli na Rais wa Congo DRC Joseph Kabila wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari Ikulu bofya hapa
Polisi Aliyerekodiwa Akipokea Rushwa Kuchukuliwa Hatua bofya hapa
Jeshi La Polisi Nchini Latoa Onyo Kali Kwa Wananchi Wanaojichukulia Sheria Mkononi. bofya hapa
Tanzania na Congo DRC zimesaini mkataba wa makubaliano kutafuta mafuta Ziwa Tanganyika bofya hapa
Mambo Muhimu Waliyoyajadili Rais Magufuli na Rais wa Congo DRC Joseph Kabila wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari Ikulu bofya hapa
Post a Comment
Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)