Mmoja ya makomando wa Uturuki waliokamatwa
Wanajeshi maalum wa Uturuki wamewatia mbaroni wanajeshi wanaoshukiwa kufanya jaribio la kumteka rais Recep Tayyip Erdogan wakati jaribio la mapinduzi lililotibuka, lilipoanza wiki mbili zilizopita.
Ripoti zinaarifu kwamba takriban makomando 11 walitiwa mbaroni nje ya mkahawa wa Marmaris ambapo rais Erdogan alikuwa ameenda likizoni, japo alitoweka baada ya kudokezewa kuhusu mpango huo kabla ya makomando hao kumvamia.
Maafisa wanasema ndege zisizokuwa na rubani na helikopta zilitumiwa kuwasaka watoro hao, baada ya kuonekana na wanakijiji wakiwinda ngiri katika eneo hilo la misitu
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu August 1, 2016 bofya hapa
Post a Comment
Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)