Mabasi kusimamisha huduma Jumatatuh



Kuanzia Jumatatu wiki ijayo hakutakuwa na usafiri wa mabasi nchi nzima, baada ya Wamiliki wa mabasi yaendayo mikoani (Taboa) kuamua kusimamisha huduma hiyo ili yafanyiwe ukaguzi na Polisi
.


Katibu Mkuu wa Taboa, Enea Mrutu amesema zaidi ya mabasi 4,000 yanayohudumia safari za mikoani, yatasimamisha huduma kuruhusu ukaguzi uliolenga kupunguza ajali za barabarani na kwamba, wameshaiandikia Sumatra barua kuitaarifu juu ya suala hilo.


“Tunataka mabasi yetu yakaguliwe kwa pamoja ili mamlaka husika zithibitishe ubora na kama yanaweza kuendelea kutoa huduma za usafiri bila wasiwasi wowote,” amesema.


Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top