IS yamtangaza kiongozi mpya wa Boko Haram

Abu Musab al-Barnawi
  Boko Haram Image caption Katika video ya Boko Haram , Abu Musab al-Barnawi ametajwa kuwa msemaji wa kundi hilo

Boko Haram

Kundi la wapiganaji wa Islamic State limetangaza kuwa kwamba tawi lake la Afrika magharibi la Boko Haram lina kiongozi mpya.

Abu Musab al-Barnawi ambaye alikuwa msemaji wa kundi hilo ndio anayeonekana kuchukua uongozi wa kundi hilo.Hatahivyo kundi halijasema nini kilichomtokea aliyekuwa kiongozi wake Abubakr Shekau.

Mara ya mwisho kusikika ni katika kanda ya sauti mwezi Agosti akisema kuwa yuko hai na kwamba nafasi yake haijachukuliwa -huku kanda ya video ya ISIS iliotolewa mwezi Aprili ikithibitisha hilo.KUndi la Boko Haram ambalo limepoteza eneo kubwa lililokuwa likidhibiti miezi 18 iliopita linapigana kuiondoa madarakani serikali ya NIgeria.

Mashambulio yake ya miaka saba yamesababisha vifo vya watu 20,000 hususan katika eneo la Kaskazini mashariki.
 

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top