OBAMA: CLINTON ANAFAA ZAIDI KUWA RAIS MAREKANI

Rais wa Marekani Barack Obama amemsifu sana mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton na kusema ndiye afaaye zaidi kuongoza Marekani.

Akihutubu katika kongamano kuu la chama cha Democratic mjini Philadelphia, huku akishangiliwa na wajumbe, Rais Obama amesema hakujawahi kuwa na mtu aliyehitimu zaidi kuongoza Marekani kuliko Bi Clinton.

"Hakujawahi kuwa na mwanamume au mwanamke, iwe mimi au Bill Clinton au mtu mwingine yeyote aliyekuwa amehitimu zaidi kuwa rais kama yeye," amesema Bw Obama.

Amemsifu pia kwa kujikakamua na kuwa mwanamke wa kwanza katika historia ya taifa hilo kuteuliwa kuwa mgombea urais wa chama kikubwa.


Obama ameshutumu sera za Donald Trump

Amempongeza kwa kubomoa vizuizi na kuunda nafasi zaidi kwa Wamarekani.

Amewaahidi Wamarekani kwamba Bi Clinton anatetea umoja na maadili ya Wamarekani.


Bw Obama pia amemkosoa vikali mgombea wa chama cha Republican Donald Trump.

Awali, Seneta wa Virginia Tim Kaine alikubali rais uteuzi wa kuwa mgombea mwenza wa Bi Clinton


 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano July 27, 2016 bofya hapaNAFASI  ZA KAZI BOFYA HAPA 


Tume ya vyuo Vikuu Tanzania( TCU) yatangaza vyuo Vikuu vilivyofungiwa BOFYA HAPA


News alet:Majina ya wanafunzi waliochanguliwa kujiunga Certificate na Diploma na NACTE 2016/2017 bofya hapa

News alert:Tume ya vyuo Vikuu Tanzania( TCU) yatangaza vyuo Vikuu vilivyofungiwa BOFYA HAPA

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top