Mikoa ya Dar es Salaam na Dodoma Yaongoza Kwa Mapenzi ya Jinsia Moja

Takwimu zilizotolewa na wizara ya afya, maendeleo ya jamii jinsia , watoto na wazee nchini zinaonyesha kuwa mkoa wa Dar es salaam na Dodoma inaongoza kwa vitendo vya mapenzi ya jinsia moja


Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam waziri wa wizara hiyo Mhe. Ummy Mwalimu alisema kutokana na hali hiyo wizara imepiga marufuku matumizi ya vilainishi vinavyotumiwa na baadhi ya makundi yanayo jihusisha na vitendo hivyo.


Mhe. Ummy Mwalimu alisisitiza kuwa serikali imeamua kuzuia vilainishi hivyo kwani vimetajwa kuchochea vitendo hivyo ambavyo nikinyume na sheria na taratibu za nchi nakuongeza kuwa vitendo hivyo nimiongoni mwa sababu inayochangia ongezeko la VVU.


Aidha Mhe. Ummy alisema kuwa kwa sasa serikali inajikita kuhakikisha kuwa inajenga wodi za wazai, kununua vifaa tiba, madawa ya kutosha katika hosptali zake na sio ununuzi wa vilainishi hivyo.

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top