Waliohamishiwa UDOM kutoka St Joseph kurudia mwaka


Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknlojia Imewataka wanafunzi wa St. Joseph walioamishiwa katika chuo kikuu cha Dodoma kurudia mwaka kwa kile kilichobainika kuwa na ujuzi na maarifa usiokidhi viwango vya chuo cha Dodoma.

Wizara hiyo pia imesema kwamba watakaogomea uamuzi huo watatakiwa kurudi makwao .


Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, katika mkutano wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania TCU, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako alisema, ni lazima wanafunzi hao warudie mwaka kwani wamepimwa na kubainika kuwa na uwezo mdogo hivyo hatua ya kuwataka kurudia mwaka ni nafasi ya pili kwao.


Prof. Ndalichako alisema, kwa sasa wizara yake inaandaa ripoti ya vyuo vinavyofundisha chini ya viwango ambapo amesema mara tu baada ya kukamilika ripoti hiyo, itatolewa na kwamba kwa wale wanafunzi ambao vyuo vyao vimefungwa kwa kutokidhi vigezo ni lazima wapimwe kiubora ili kupata wanafunzi watakao kidhi vigezo vya soko la ajira.


Aidha, Prof. Ndalichako ametoa onyo kwa wanafunzi ambao wamegushi nyaraka mbalimbali ikiwemo za vifo vya wazazi wao ama ugonjwa na kufanikiwa kupata mkopo wa elimu ya juu kwa njia ya udanganyifu kuwa wizara hiyo inafanya uhakiki na pindi watakapo bainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
 

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top