Mbunge Mwingine wa CHADEMA Atiwa Mbaroni




Mbunge wa Ukonga kwa tiketi ya Chama cha Demokrsia na Maendeleo (CHADEMA), Mwita Waitara anashikiliwa na Polisi katika kituo cha Polisi Chang’ombe, Temeke, Dar es Salaam.


Mbunge Waitara amekamatwa jana alipokuwa katika eneo la Uvikiuta alikokwenda kufuatilia mgogoro wa ardhi wa muda mrefu kati ya wananchi wa eneo hilo na anayedaiwa kuwa kigogo wa serikali anayetuhumiwa kuwa anataka kupora ardhi hiyo na kuwahamisha wananchi kwa nguvu.


Mbunge huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Kivule alifika katika eneo hilo lenye mgogoro ambapo shughuli ya kubomoa nyumba 500 za wananchi wa eneo hilo ilikuwa ikiendelea.


Eneo lenye mgogoro lipo mpakani mwa wilaya za Ilala na Temeke (Kivule-Ilala na Mbande-Temeke). 
 

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top