Ushindani wa usafiri wa anga kuongezeka, siku chache tu baada ya serikali kuleta ndege mpya,Fasjet nao kuagiza ndege mpya



.
 Kampuni ya ndege ya Fastjet imepanga kuingiza nchini ndege moja jamii ya Embraer 190 ili kukabiliana na hali ngumu ya sasa ya kibiashara
.


Jana Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, John Corse amesema ndani ya wiki mbili zijazo wataingiza ndege mpya katika safari zake ikiwa ni sehemu ya majaribio ya kutekeleza mkakati wa mabadiliko.


“Tunatarajia ndege hiyo itakuwa jamii ya Embraer 190 na itafanya kazi kwa mujibu wa kanuni ya ‘waitlist’. Baada ya kufanya uchambuzi wa kina tulibaini aina hii ya ndege zinaendana na mazingira ya kibiashara ya sasa,” amesema Corse.


Amesema mchakato wa kubadilisha aina ya ndege utafanyika polepole na huenda ukachukua zaidi ya miezi sita ili kuendana na mahitaji ya sera na sheria za udhibiti wa mawasiliano ya anga nchini.


 Habari zilizopo katika magazeti ya leo ijumaa september 23, 2016 bofya hapa

Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top