Akamatwa kwa kupanda mnara wa makao makuu ya Trump Marekani



Polisi wakijitahidi kumuondoa

Mtu mmoja aliyejaribu kupanda mnara wa Trump uliopo jijini New York, ameondolewa na polisi katika jengo hilo baada ya kuchomwa na vioo vya jengo hilo lenye ghorofa hamsini na nane ambayo ni makao makuu ya kampeni za kumchagua Donald Trump.
Mpandaji alionekana amelewa

Trump anaishi kwenye chumba cha juu ya ghorofa hilo lakini kwa sasa anafanya kampeni zake nje ya mji.

Mpandaji alijivuta huku akiwa akionekana kuwa amelewa, akitaka kuingia ndani ya jengo hilo.
Umati wa watu ukishuhudia polisi wakimuondoa

Polisi waliofika eneo la tukio wamesema hawakuweza kutambua nini haswa lilikuwa lengo lake.

Hatimaye polisi walifanikiwa kumuingiza ndani ya jengo hilo


 Ajira Zaidi bofya hapa

Magazeti ya leo alhamisi August 11, 2016 bofya hapa









Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top