Serikali Yakanusha Kuwepo Kwa Ugonjwa wa ZIKA Nchini


WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imesema hakuna uthibitisho wa kuwepo kwa ugonjwa wa Zika nchini.
Imeeleza kuwa utafiti uliofanyika
ni wa kuangalia ubora wa kipimo cha ugonjwa huo.
Ufafanuzi wa Wizara hiyo umekuja siku moja baada ya Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kutoa ripoti ya utafiti uliofanywa na taasisi hiyo kwa kushirikia na Chuo Kikuu cha Kanisa Katoliki Bugando, inayoeleza kuwepo wa maambukizi ya virusi vya Zika katika jamii ya Watanzania.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alitoa ufafanuzi huo kwa waandishi wa habari jana, ambapo alisema wananchi wanapaswa kuondoa hofu kwa kuwa ugonjwa huo haujaingia nchini.
“Napenda kuwatoa hofu wananchi kwa sasa haijathibitishwa kuwepo kwa ugonjwa wa Zika nchini…wao walifanya utafiti nchini wa kuchunguza ubora wa kipimo cha kupima magonjwa ya Zika na Chikungunya, hawakupima kama zika ipo nchini au hakuna,” alisema Waziri Ummy.
Alisema wizara yake itaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali, kutafiti ili kubaini kama ugonjwa wa Zika upo nchini au la.
Wizara hiyo pia imeshaanda mkakati wa Zika nchini, unaoelekeza kufuatilia ugonjwa huo.
Mganga Mkuu wa Serikali, Mohammed Kambi alisema, NIMR walichokifanya ni kufanya utafiti wa kutathmini ufanisi na ubora wa kipimo, ambacho kinaweza kuja kutafiti magonjwa ya zika na mengine na kwamba kiutaratibu hizo ni hatua za awali.
Alisema, taarifa hiyo ya NIMR itafanyiwa tathmini ya kisanyasi ili wanasayansi wajiridhishe kama ilifuata taratibu zote na matokeo hayo yanaweza kuendelezwa mbele zaidi na baadae kuweka mikakati ya kuzidi kuthibisha uwepo wa ugonjwa huo.
“Tuna taratibu hizo za upande wa kitaalamu lakini kuna taratibu katika kutoa tamko, kuhusu uwepo wa ugonjwa kama huu kwasababu ni aina ya uginjwa unaotakiwa uripotiwe kimataifa…inabidi taarifa ije rasmi katika wizara, kuna mganga mkuu na Shirika la Afya tuangalie hizo na tukijidhihirisha taarifa rasmi inatolewa na mratibu wa magonjwa hayo,” alisema Dk Mohammed.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa NIMR, DK Mwele Malecela alisema taarifa aliyoitoa juzi, ilikuwa ni matokeo ya utafiti wa kubainisha uwezo wa kipimo hicho katika kuanisha virusi vya Zika, Dengue na Chikungunya na matokeo ya awali yalionesha uwepo wa virusi vya Zika.
Alisema pamoja na matokeo hayo, hawakuona dalili wala madhara yoyote yanayosababishwa na Zika ikiwemo Kichwa kidogo na mengine.
“Hili suala ni kwamba lilikuwa ni suala la kuainisha na katika uanishaji huo tukajikuta tumeona virusi hivyo, lakini hiyo haimanishi kuna uthibitishio, naomba nisisitize uthibitisho wa ugonjwa unatolewa na wizara ya afya kwa kufuata uatartibu maalumu uliowekwa,” alisema.
Alisema kuwa wataendelea kufanya utafiti hasa katika kuangalia magonjwa ya Zika, Dengue na Chikungunya na kutoa matokeo kwa kile watakachokipata katika utafiti huo.
Juzi NIMR ilitoa matokeo ya utafiti uliofanywa na taasisi hiyo pamoja na Chuo Kikuu cha Katoliki cha Bugando na utafiti kuanisha uwepo wa maambukizi ya virusi vya zika katika jamii ya Watanzania na kuangalia adhati ya maambukizi katika kusababisha watoto wanaozaliwa na ulemavu.
Sampuli za damu kutoka kwa watu 533 zilipimwa. Kati yao, watoto wachanga 80 walizaliwa na ulemavu wa viungo mbalimbali. Kati ya waliopimwa 533, 83 (15.6%) waligundulika kuwa wameambukizwa virusi vya Zika.
Kati ya wale watoto wachanga 80 waliozaliwa na ulemavu, 43.8% walikuwa wameambukizwa virusi vya Zika, utafiti unaendelea kujua ukubwa wa tatizo hili.


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi December 17, 2016 bofya hapa 



Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top