Majambazi Hatari Wauawa Bunduki 9 Zakamatwa

Jeshi la polisi limedai kwamba limeua majambazi wawili hatari na kukamata bunduki tisa, kati ya hizo SMG saba, shotgun moja na riffle moja, risasi 473 na magazini 16 baada ya majibizano ya risasi katika misitu ya Milima ya Usambara, Kijiji cha Magamba wilayani Lushoto.


Katika majibizano hayo, pia polisi walidai kukamata bendera zenye maandishi ya lugha ya Kiarabu, redio saba za upepo na soksi za kuficha nyuso.

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Polisi, Nsato Marijani alisema jana kuwa hiyo ilikuwa operesheni ya kuwasaka majambazi waliovamia Chuo Kikuu cha Sekomu, wilayani humo hivi karibuni.


Alisema katika tukio hilo, askari wawili walijeruhiwa kwa risasi. Marijani ambaye alikuwa katika milima hiyo inayodaiwa kuwa ngome ya majambazi hao, aliwataja waliouawa kuwa ni Mudrick Abdi (24) maarufu kwa jina la Osama, mkazi wa Mbagala Majimatitu Dar es Salaam na Sultan Abdallah (24) mkazi wa Kiembesamaki, Zanzibar.


Alisema askari waliojeruhiwa wanaendelea na matibabu na kwamba hawakupata madhara makubwa kwa kuwa walikuwa wamevaa majaketi ya kuzuia kupenya risasi . 
 
 




Like page yetu ya facebook upate habari kwa urahisi na haraka zaidi BOFYA HAPA


Post a Comment

Toa maoni tu (kejeli na matusi marufuku)

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top