Wabunge Waionya Serikali

WABUNGE wameonesha wasiwasi kuhusu kupunguzwa kwa fungu la fedha katika Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali na kuonya kuwa huenda hatua hiyo ikampunguzia Rais John Magufuli kasi ya utumbuaji majipu, anayoifanya kwa wabadhirifu wa fedha za umma au kuua kabisa utaratibu huo.


Wabunge hao walionesha wasiwasi huo kwa nyakati tofauti bungeni mjini hapa Dodoma, wakati wakichangia hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2O16/17 inayoanza kutekelezwa Julai mosi, mwaka huu.


Miongoni mwa wabunge hao ni wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM), aliyeeleza kuwa, kupunguza fedha katika ofisi hiyo ni kumkwamisha Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya kazi yake kwa ufanisi na tija.


Kwa mujibu wake, kumkwamisha huko pia ni dalili ya kuukumbatia ufisadi kwa sababu ofisi hiyo ya CAG ndio inayofanya kazi ngumu na kubwa ya kuwafichua mafisadi nchini, hivyo inahitaji kujitosheleza kibajeti na kuepuka kuhitaji msaada kutoka kokote kwingine.


“Kitendo cha kuminya fungu la ofisi ya CAG kwa kupunguza kiasi cha fedha inachopewa kutoka shilingi bilioni 74 kwa mwaka wa fedha unaoisha hadi shilingi bilioni 44 kwa mwaka mpya wa fedha unaoanzia Julai Mosi, ni kuifanya ofisi hiyo ishindwe kuyabaini majipu (wabadhirifu, mafisadi),” Lugola alisema.
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top