Mtihani wa Marekani wafutwa Korea Kusin na Hong Kong

Chuo kikuu cha California nchini Marekani

Mtihani unaowapa nafasi wanafunzi wa kigeni kuingia katika vyuo vikuu vya Marekani umefutwa nchini Korea Kusini na Hongkong baada ya vifaa vya mtihani huo kuibwa.

Mtihani huo umefutwa saa chache tu kabla ya wanafunzi zaidi ya 5000 kutahiniwa.

Mtihani huo, unaotolewa na shirika la Marekani la ACT unatumiwa na vyuo vikuu vya Marekani kutathmini wanafunzi wa kimataifa.

Kila mwaka, maelfu ya wanafunzi huwa wanaomba nafasi ya kusomea vyuo vikuu vya Marekani.
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top